SUMAJKT AGRI-BUSINESS COMPANY LTD

Huduma Zetu

Kilimo

Shughuli za uzalishaji kupitia kilimo zinaendeshwa kwenye maeneo mbalimbali ya Makambi na vikosi vya JKT. Kwa sasa, shughuli hizi husimamiwa na mameneja kwenye maeneo husika tofauti na hapo awali ambapo makamanda vikosi walikuwa wakisimamia shughuli hizo. Shirika linaendelea kupanua shughuli za kilimo kwa kutafuta mashamba mapya na yale yanayotolewa na Serikali kupitia Ofisi ya Msajili wa Hazina (TR) kwa lengo la kuyaendeleza kibiashara.

Ufugaji

SUMAJKT Cleaning and Fumigation Company Limited offers guaranteed fumigation and pest control solutions to types of customers nationwide. The most effective method used for controlling pests is fumigation.

Our fumigation and pest control services are highly effective in exterminating and getting rid of rodents, mosquitos, bedbugs, termites and ants, among others in homes, offices and schools. We are the exceptional choice for our customers in need of fumigation and pest control services.

Uvuvi na Ufugaji Samaki

Kwa sasa Shirika linaendesha shughuli za ufugaji katika baadhi ya makambi na vikosi vya JKT. Kwa kuzingatia mkakati wa JKT kujitosheleza kwa chakula na Shirika kujiendesha kibiashara, mgawanyo wa rasilimali mifugo ulifanyika mwaka 2017 katika shamba la Mifugo Oljoro (833 KJ) Mkoani Arusha. Shamba hili linafuga ng’ombe wa nyama na maziwa na shamba la mifugo Mafinga (841 KJ) Mkoani Iringa, ambalo huzalisha maziwa pamoja na kufanya biashara ya kuuza mitamba. Aidha, Shirika linafuga katika Huria ya Misenyi ndani ya Kiteule cha Misenyi mkoani Kagera ambapo linafuga ng’ombe wa nyama aina ya Ankole, mbuzi na kondoo. Shirika linaboresha na kufuga kitaalamu ili kukidhi mahitaji ya soko.

Agri-Machinery

Mradi huu umekuwa msaada kwa wakulima tangu kuanzishwa kwake kwani wengi wamefaidika kupitia huduma ya Matrekta na zana zake. Aidha, huduma ya kusambaza matrekta, zana na vipuri vyake umesaidia kuanzisha mradi wezeshi wa kuuza matrekta, vipuri na zana za kilimo kwa njia ya fedha taslimu. Matrekta na zana hizo ni; Matrekta ya New Holland na FARMTRAC, majembe ya kulimia (Disc Plough), jembe la kuvunja udongo (Disc harrow), pump za umwagiliaji (Irrigation water pump) na tela (Trailer).

Mradi huu umewawezesha wakulima nchini kufaidika kwa kupata uelewa wa matumizi juu ya zana za kilimo, kuongeza uzalishaji wa mazao ya kilimo na ajira hasa maeneo ya vijijini. Pia, mradi unatekelezwa kwa kukusanya madeni kwa watu na taasisi zilizopewa Matrekta na vipuri.
SUMAJKT AGRI-BUSINESS COMPANY LTD© 2023 | Imewezeshwa na Kutengenezwa na SUMAJKT
linkedin facebook pinterest youtube rss twitter instagram facebook-blank rss-blank linkedin-blank pinterest youtube twitter instagram